Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Featured Posts

Tuesday, June 28, 2016

SERIKALI YATAKIWA KUKAMILISHA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA SONGWE.

 
Meneja wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uliopo mkoani Mbeya, Hamis Amir akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari kutoka TAJATI (hawapo pichani).

Meneja wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uliopo mkoani Mbeya, Hamis Amir akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari kutoka TAJATI.

Meneja wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uliopo mkoani Mbeya, Hamis Amir akiwatembeza Waandishi wa habari kutoka TAJATI.

Meneja wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uliopo mkoani Mbeya, Hamis Amir akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari kutoka TAJATI

Jengo la abiria ambalo halijakamilika.

Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Kanda, Issa Hamad akitoa maelezo kwa Wana TAJATI.

Muonekano wa majengo katika uwanja wa ndege Songwe

Muonekano wa Uwanja wa ndege wa Songwe.

Senior Breafing officer wa Songwe airport akifafanua jambo

Muongoza ndege Bertila Ngowi akitoa maelezo na changamoto zinazowakabili. 
 
ILI kuongeza idadi ya Wawekezaji na Watalii kwa Mikoa ya Nyanda za Juu kusini, Serikali imetakiwa kukamilisha mara moja ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Songwe uliopo mkoani hapa.
 
Imeelezwa kuwa ikiwa uwanja huo ukimaliziwa idadi kubwa ya Watalii na ndege kubwa zitaweza kutua na kuongeza  wawekezaji na kutoa fursa za kiuchumi kwa wakazi wa mikoa ya nyanda za juu.
 
Wito huo ulitolewa na Kaimu Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, Hamisi Amiri,alipokuwa akizungumza na Wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji nchini(TAJATI)katika mwendelezo wa ziara zake nchini kuibua fursa za utalii na uwekezaji.
 
Amiri alisema hivi sasa uwanja huo unakabiliwa na Changamoto ya Jengo la kufikia abiria ambalo ujenzi wake umekwama kwa muda wa mwaka mmoja sasa kutokana na ukosefu wa fedha.
 
“jengo la kufikia abiria limekwama kuendelea na ujenzi kwa zaidi ya mwaka mmoja hivi sasa kutokana na serikali kukosa fedha za kumlipa mkandarasi zaidi ya shilingi bilioni kumi na moja kazi ambayo ingemalizika kwa kipindi cha miezi sita kama pesa zingekuwepo”alisema Meneja huyo.
 
Alisema  Serikali imetoa pesa kwa ajili ya ufungwaji wa taa katika njia ya kurukia ndege hivyo kuondoa adha ambayo wanakumbana nayo marubani wakati wa kutua na kuruka pindi kunapotokea hali ya mawingu katika uwanja huo ambao upo kwenye ukanda wa bonde la ufa.
 
Kwa upande wake Afisa usafirishaji wa abiria katika uwanja huo Jordan Mchami alisema kukamilika kwa jengo la abiria kutasaidia kuongezeka kwa mashirika mengine ya ndege ya kimataifa na kuongezeka kwa abiria na kwamba jengo hilo linaweza kupokea abiria zaidi ya elfu moja kwa wakati mmoja.
 
Baadhi ya waongozaji wa Ndege katika uwanja huo walisema  changamoto kubwa inayo wakabili katika uwanja huo ni pamoja na marubani kukumbana na  hali ya ukungu na ukosefu wa taa katika barabara ya kurukia ndege ambapo mara kadhaa ndege zimekuwa zikishindwa kutua kwa wakati na  pengine kurudi zilikotoka kutokana na hali hiyo.
 
Katika hitimisho la ziara hiyo Meneja wa Uwanja wa Ndege Amiri Hamisi alisema  waandishi wa Habari wana nafasi kubwa katika mchango wa uchumi kama ambavyo wameweza kuokoa uwanja mdogo wa zamani uliopo Kata ya Iyela uliokuwa umevamiwa na baadhi ya viwanja kuuzwa na baadhi ya wananchi kwa kushirikiana na mamlaka za umma.
 
Amiri alisema Waandishi baada ya kuitoa habari hiyo Serikali imetoa shilingi milioni mia sita(600,000/=) kwa ajili ya upimaji na umiliki kisheria ili kuzuia uvamizi ikiwa ni pamoja na kuweka uzio kwa ajili ya usalama ili kuzuia mifugo na watu wanaokatiza uwanjani pindi ndege zinapotua na kuruka katika uwanja wa ndege wa Songwe.
 
Ziara hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Ulimboka Mwakilili ilitembelea huduma mbalimbali katika uwanja huo kama Idara ya Utabiri wa Hali ya Hewa,Kikosi cha Zimamoto na uokoaji,Uongozaji wa Ndege na Huduma za usafirishaji wa abiria.
 
Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka wa Hali ya Hewa,Kanya ya Nyanda za juu kusini, Issah Hamadi alisema Idara hiyo ina vituo mbalimbali vya utabiri wa hali ya hewa ambavyo husaidia katika shughuli za anga na Kilimo na kwamba kituo hicho kilianzishwa mwaka 1929.
 
Issah alisema kituo hicho ambacho hufanya shughuli zake uwanja wa ndege wa zamani na Songwe kimepata tuzo ulimwenguni kutokana na huduma bora za utabiri wa hali ya hewa hivyo kuleta heshima kwa Taifa kutokana na utendaji wake bora.

Friday, June 24, 2016

TIBA YA MAGONJWA YAKO NA MATATIZO MBALIMBALI SASA HII HAPA BEI NAFUU SOMA HAPA KWA MAKINI

Je?  Unaumwa au unasumbuliwa na matatizo  yoyote kiafya? Unahitaji msaada wa haraka, tuna virutubisho sahihi kuondoa magonjwa kama kisukari, presha, uvimbe, magonjwa ya ngozi,mifupa, mgongo,  kansa, matatizo ya uzazi, vidonda vya tumbo na mengineyo mengi usisite kututafuta.
Tupo magomeni mwembechai
Piga: 0715908307.
Whatsapp :0754-908307.

Bei ni nafuu afya ni muhimu.
Je?  Unaumwa au unasumbuliwa na matatizo  yoyote kiafya? Unahitaji msaada wa haraka, tuna virutubisho sahihi kuondoa magonjwa kama kisukari, presha, uvimbe, magonjwa ya ngozi,mifupa, mgongo,  kansa, matatizo ya uzazi, vidonda vya tumbo na mengineyo mengi usisite kututafuta.
Tupo magomeni mwembechai
Piga: 0715908307.
Whatsapp :0754-908307.

Bei ni nafuu afya ni muhimu.

Tuesday, June 21, 2016

CHUO KIKUU TEKU CHAJIPANGA KUPUNGUZA TATIZO LA AJIRA KWA KUONGEZA WASOMI

 
Wahitimu wa fani mbali mbali wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Chuo kikuu cha TEKU baada ya kumalizika kwa Mahafali ya 9 yaliyofanyika juzi chuoni hapo

Baadhi ya Wazazi jamaa na marafiki waliojumuika pamoja na Wahitimu wa Diploma ya Habari na mawasiliano kwa umma wakiwa katika picha ya pamoja

Wahitimu wakiwa ukumbini wakifuatilia kwa makini matukio yanayoendelea

Baadhi ya Wahitimu wa Fani ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya uuma wakiwa katika picha ya pamoja

Wahitimu wa Fani ya Uandishi wa habari wakifurahia jambo baada ya kumaliza sherehe za mahafali, Wa kwanza kulia ni Godfrey Kahango kutoka gazeti la Mwananchi Mbeya.

Baadhi ya Ndugu wakiwa katika picha ya pamoja na wahitimu Godfrey Kahango na Rogate Andrew

Godfrey Kahango akiwa katika pozi

Godfrey Kahango akifurahia kulishwa keki na dada zake akiwemo Amina Said kutoka Star Tv Mbeya (Kulia)

Godfrey Kahango akilishwa keki na Venance Matinya ikiwa ni Ishara ya kumpongeza kwa kumaliza masomo yake ya uandishi wa Habari na Mawasiliano ya umma katika ngazi ya Diploma
ILI   kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana na wahitimu wa fanimbali mbali nchini, Uongozi wa Chuo kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) kilichopo jijini Mbeya umejipanga kuhakikisha unaongeza kozi chuoni hapo.
 
Akitoa taarifa ya kurugenzi ya Elimu Anuai ya Chuo Kikuu cha TEKU, Kaimu Mkurugenzi, Simwaba Joseph alisema chuo kinatarajia kuongeza programu za uuguzi, ualimu wa Sekondari na Msingi kwa mwaka wa masomo wa 2016/2017  ili kusaidia vijana wengi kujinasua kutoka katika wimbi la ukosefu wa ajira.
 
Kaimu Mkurugenzi huyo alitoa taarifa hiyo juzi katika sherehe za Mahafali ya Tisa ya Chuo hicho zilizofanyika katika Ukumbi wa mikutano uliopo Block T jijini Mbeya ambapo wahitimu walitunukiwa Shahada katika fani mbali mbali ikiwemo Uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma.
 
Joseph alisema katika Mahafali hayo jumla ya wanafunzi 191 waliajiandikisha lakini hadi wanahitimu ni  wanafunzi 157 watapewa shahada kutokana na fani walizosoma, na wanafunzi 34 hawajaweza kuhitimu mafunzo yao kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za wengine kushindwa kulipa ada.
 
Awali Akisoma risala ya wahitimu hao, Lwiza John, aliyesoma fani ya Uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma aliuomba uongozi wa chuo hicho kupunguza kiwango cha ada kwa kuwa imekuwa ni mzigo kwao.
 
"Kiwango cha ada ni kikwazo kwetu na tunaomba uongozi ulifikirie hili ili ada kwa mwanafunzi wa astashahada ipungue kutoka Sh700,000 hadi 600,000 na stashahada ipungue kutoka 900,000 hadi 800,000," alisema Lwiza.
 
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Tully Kasimoto aliiomba Serikali kuondoa utitiri wa kodi wanazotozwa kwa shule na vyuo  binafsi,hali ambayo wamedai kuwa inadumaza utendaji kazi wao kwa kushindwa kuboresha huduma hiyo muhimu kwa jamii.
 
Alisema vyuo binafsi vinatozwa kodi nyingi tofauti na vyuo vya serikali hali inayowapa wakati mgumu wamiliki hao na kupelekea wanafunzi kulalamikia ukubwa wa ada pasipokujua kuwa sababu ni mlundikano wa kodi.
 
Alisema lengo la wamiliki wa vyuo na shule binafsi ni kutoa huduma kwa vijana na siyo kufanya biashara na kwamba wanashindwa kuboresha mazingira ya elimu kwa vijana kutokana na fedha nyingi kutumika katika ulipaji wa kodi.
 
"Suala la kodi ni changamoto kwetu kwani tunatoa kodi nyingi tofauti na vyuo vya serikali na hili linadumaza utendaji kazi wetu kutokana na sisi tuna lengo la kutoa huduma kwa vijana na siyo kwamba tunafanya biashara, "alisema Kasmoto.
 
Kuhusu udahili wa wanafunzi wasiokuwa na sifa ya kujiunga na vyuo, Kasmoto alisema suala hilo linapaswa kuangaliwa kwa umakini kwani wanaodahili wanafunzi hao wamekosa uaminifu na hawana nia nzuri ya kukomboa vijana.
 
"Hivi sasa serikali ndiyo inasimamia suala hilo la udahili wa mfumo wa pamoja na ili kuhakikisha vyuo havidahili wanafunzi hewa ni vyema mfumo uchunguzwe upya na hata hivyo mwanafunzi huyu kwa vyovyote vile atashindwa kufanya vizuri kwenye mitihani yake, "alisema.
 

Monday, June 20, 2016

Maadhimisho ya mtoto wa Africa yafana Mbeya

Maadhimisho ya mtoto wa Africa na uzinduzi wa mkakati wa Dream utakaodumu kwa kipindi cha miaka miwili wenye lengo la kusaidia kupambana na ongezeko la maambukizi ya ukimwi na mkoa ni wa tatu baada ya Njombe na Dar. Mwakilishi wa tume ya kudhibiti ukimwi nchini Tacaids EMMANUEL Petro amesema kuwa mpango wa kudhibiti maambukizi utasambazwa nchini kote na kwa kuanzia wameanza na mikoa mitatu nchini ya Dar Shinyanga Mbeya na Wilaya saba zitanufaika na mkakati huo ambao utasaidia kutoa elimu kwa wahanga ili kujitegemea kwa kuwawezesha kiuchumi na kulipa karo kwa wanafunzi ili wawe salama kiafya waweze kutimiza ndoto zao za kimaisha. Kaimu mganga mkuu wa Mkoa wa mbeya Agnes Buchwa ameishukuru serikali ya Marekani kwa kusaidia juhudi za kupambana na maambukizi ya ukimwi  mkoa wa Mbeya.






Wednesday, June 15, 2016

Waendesha bodaboda watakiwa kufuata Kanuni,Sheria na Taratibu za Barabarani Jijini Mbeya.

Na Daudi Manongi,MAELEZO.

Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya Bw.Godlove Mbwaji amehaidi kufanya kikao na uongozi wa waendesha bodaboda wa mkoa wa mbeya ili kuzungumzia suala la waendesha pikipiki hao kuvamia hospitali hiyo wakiwa katika kundi kubwa wakati wanapofiwa na dereva mwenzao na kusababisha usumbufu kwa wagonjwa na wakazi wa mbeya.

Mkurugenzi uyo ametoa rai kwa waendesha bodaboda hao kuwa na nidhamu wanapoingia katika hospitali hiyo kwani inatumiwa na wakazi wote wa Jiji la Mbeya na husababisha hatari kwa wagonjwa wanaohitaji huduma ya dharura hospitali hapo kwani huziba barabara yote.

Aidha ameuomba uongozi wa waendesha bodaboda hao kuchagua watu wachache wanapokuja kuchukua mwili wa mwenzao kwani itasaidia kupunguza kelele za honi na vyombo vyenyewe kwani pia kuna majirani wanaokaa katika eneo hilo wanatumia barabara hizo na hivyo kuepusha ajali.

Pia Bw.Mbwaji ametoa ushauri kwa uongozi wa waendesha bodaboda hao kuacha vitendo vya uvunjifu wa sheria na wafuate Sheria,Kanuni na taratibu za Barabarani pale mmoja wapo anapokamatwa au kugongwa kwa kutojicjhukulia sheria mkononi kumpiga aliyemgonga au kuwafanyia fujo polisi kwa kumvamia muhusika wakiwa katika makundi makubwa na hivyo kuhatarisha usalama wa Raia.

Aidha baadhi ya madereva bodaboda wa mkoa huo wamesema kuwa wamekuwa wakishinikizwa na viongozi wa matawi yao kwa madai kuwa atakayekataa kwenda kwenye maandamano atatozwa faini ya sh.50000, hata kama amebeba abiria ulazimishwa kumshusha.

COCA-COLA KUENDELEA KUDHAMINI MASHINDANO YA UMISSETA NCHINI TANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makalla akikagua wachezaji wakati wa Uzinduzi wa mashindano ya UMISETA ambayo mwaka huu yamedhaminiwa na kampuni ya Coca Cola. Uzinduzi huo ulifanyika May 10, 2016 katika uwanja wa Sokoine ambapo kulifanyika michezo na burudani mbali mbali. --- Mashindano kwa ajili ya fainali za kitaifa za Copa-UMISSETA ambayo yanadhaminiwa na kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola, na ambayo yalipangwa kuanza kufanyika siku ya leo hadi hapo tarehe 24 Juni 2016 yametangazwa kuahirishwa. Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya serikali iliyotolewa hapo jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), George Simbachawene, serikali imechukua uamuzi huo ili kupisha utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli la upatikanaji wa madawati, ambao kikomo chake ni mwisho wa mwezi huu. Mashindano haya ya fainali za Copa-UMISSETA yalilenga kuzikutanisha timu za mikoa mbalimbali nchini kwa pamoja Jijini Mwanza, zikiwa zimeundwa na wachezaji mbalimbali kutoka shule za sekondari ili wachuane kwenye michezo na sanaa.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke - Dar es Salaam, Sophia Mjema (kushoto), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Makongo Sekondari katika Mashindano ya UMISETA ambapo kampuni ya Coca Cola ndiyo walikuwa ni wadhamini wakubwa wa michuano hiyo kwa mwaka 2016. --- “Thamira yetu katika kudhamini mashindano haya na kushirikiana TAMISEMI iko pale pale, tukiwa tumejidhatiti kuendelea kuunga mkono jitihada za kutambua na kuinua vipaji vya vijana ambao watakuja kuifikisha Nyanja ya michezo nchini katika kiwango cha juu zaidi. Tutaendelea kuunga mkono na kusaidia kukua kwa sekta ya michezo nchini, hususani mashindano ya mpira wa miguu pamoja na mpira wa kikapu kwa vijana,” alisema David Karamagi, Mwakilishi Mkazi wa Coca-Cola Tanzania. Karamagi aliongeza kuwa kampuni ya Coca-Cola Tanzania inayo imani ya dhati na ikiamini ya kwamba mashindano ya michezo yanayoanzia ngazi ya chini kabisa ndiyo namna thabiti nay a kipekee katika kuibua vipaji vya wachezaji nchini. Pia Karamagi alisema kuwa, wakati wadau wakisubiri kwa hamu kutangazwa kwa tarehe mpya za kurejewa kwa fainali za mashindano haya nchini, Coca-Cola Tanzania ilishajipanga kudhihirisha ya kwamba michezo ni zaidi ya ushindani, kwa kuweza kuambatanisha mashindano haya na kujenga mshikamano wa timu shindani, urafiki na hata nidhamu kwa wachezaji na timu za mikoa inayoshiriki. Hivyo basi, kwa udhamini ulioingiwa mwaka huu, Coca-Cola Tanzania itaweza kupanua wigo wa ushirikishwaji wa michezo murua zaidi mbali ya mpira wa miguu, hasa kwa kuweza kujumuisha mpira wa kikapu. “Kampuni ya Coca-Cola nchini tutaendelea na dhamira yetu ya kuunga mkono jitihada ya vijana mbalimbali nchini kote katika kuwasaidia kudhihirisha vipaji vyao kupitia mashindano mbali mbali ya michezo, ikiwa ni pamoja na UMISSETA na Copa Coca-Cola’” alimalizia Karamagi.

Tuesday, June 14, 2016

MAANDALIZI YA UZINDUZI WA MRADI WA DREAMS - "BINTI JASIRI" RUANDA NZOVWE JIJINI MBEYA YAKAMILIKA

Field Officer kutoka Shirika la Kihumbe, Salha Salim akitoa taarifa juu ya upokeaji na namna ya kutekeleza Mradi wa DREAM Kulia ni Mwandishi wa habari akisikiliza kwa makini.

Baadhi ya Wajasiliamali wakiendelea na maandalizi ya kupanga bidhaa zao

Watekelezaji wa Mradi wa DREAM wakiendelea na shughuli ya uelimishaji



Wajasiliamali kutoka Shirika la Anglican wakiwa wamepanga bidhaa zao kwa ajili ya maonesho



Muonekano wa Mabanda ya maonesho katika Uwanja wa Shule ya Msingi RuandaNzovwe jijini Mbeya.


MAANDALIZI ya Sherehe za siku ya mtoto afrika sambamba na uzinduzi wa Mradi wa DREAMS inatayofanyika kimkoa katika viwanja vya RuandaNzovwe jijini Mbeya Juni 16, mwaka huu yamekamilika kwa asilimia kubwa..


Katika maadhimisho na Uzinduzi huo, Waziri Afya Jinsia,Wazee na watoto, Ummy Mwalimu anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi.


Mradi wa  DREAM wenye lengo la kutoa elimu kwa wasichana kuanzia miaka 15 hadi 24 kuhusu maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi utakaotekelezwa kwa miaka 2.


Akizungumzia maandalizi ya uzinduzi wa Mradi huo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Graciano Kunzugala alisema hadi sasa washiriki wamefika eneo la tukio na kupanga bidhaa zao.


Alisema siku ya maadhimisho na Uzinduzi wa Mradi wa DREAM unaofadhiliwa na Walter Reed Program(WRP) na kutekelezwa na Mashirika ya Kihumbe na Anglican utakuwa na manufaa kwa watoto wa kike walio kwenye hatari ya kupata maambukizi ya Virusi vya ukimwi.


Kunzugala alisema Hamasa kubwa imetolewa kwenye mashirika ya Umma, Mashirika binafsi, Shule za Msingi hadi Vyuo vikuu ambapo sherehe hizo zitapambwa na maonesho mbali mbali kutoka kwa wajasiliamali a Jiji la Mbeya.


Aliongeza kuwa sambamba na maonesho ya wajasiliamali pia Burudani zitatolewa ikiwemo Mpira wa Miguu utakaozihusisha timu za Wasichana wenye Umri kati ya Miaka 15 hadi 24 kati ya Uyole na RuandaNzovwe.


Alisema pia Elimu kuhusiana na afya na Ukimwi  itatolewa, huduma za ushauri na upimaji pamoja na Elimu ya Ujasiliamali itakayotolewa na Mashirika ya Kihumbe na Anglikan.


Alisema katika Sherehe hizo ambazo zitatanguliwa na Maandamano makubwa yatakayoanzia Soweto hadi katika Viwanja vya RuandaNzovwe ambako yatapokelewa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri Ummy Mwalimu.


Kwa Upande wao Watekelezaji wa Mradi huo, Shirika la Kihumbe walisema wameupokea vizuri Mradi wa DREAM na wajipanga vizuri kuhakikisha wanautekeleza kama walivyopangiwa na muda muafaka.


Afisa wa Kihumbe, Salha Salim alisema maeneo waliyopewa na kuyafanyia kazi ambayo tayari wameanza ni kuwatafuta na kuwatambua walengwa wa Mradi ambao ni Wasichana waliokati ya miaka 15 hadi 24. 


Aliwataja walengwa hao kuwa ni wasichana waliokwenye hali hatarishi kama walioolewa kwenye umri mdogo, wanaokuwa wakuu wa kaya na aliyefanyiwa ukatili wa kijinsia.


Aliongeza kuwa Shirika litawapatia watu hao huduma zote zinazohitajika ndani ya Jiji la Mbeya ikiwa ni pamoja na Elimu ya Ujasiliamali,elimu ya makuzi, Ushauri nasaha na upimaji wa hiari.


Mwisho.

Monday, June 13, 2016

UVCCM MBEYA WATOA TAMKO KUMUUNGA MKONO NAIBU SPIKA WA BUNGE DK. TULIA ACKSON MWANSASU.



 
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM(UVCCM)Mikoa ya Songwe na Mbeya, Amani Kajuna akisoma tamko la kumpongeza Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson Mwansasu katika kikao kilichofanyika ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Wilaya ya Mbeya mjini ya CCM,Charles Mwakipesile akichangia jambo wakati Umoja wa Vijana wa CCM wakitoa tamko la kumpongeza Naibu Spika.

Mjumbe mstaafu wa Halmashauri kuu ya Wilaya ya Mbeya mjini CCM, Mama Mwaipasi akitoa ya moyoni kuhusu kinachoendelea bungeni mjini Dodoma kwa Wabunge wa upinzani kususia vikao vya bunge



Baadhi ya Wanachama wa CCM Mkoa wa Mbeya wakifuatilia tamko likisomwa na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya na Songwe. 

TAMKO LA UVCCM MKOA WA MBEYA & SONGWE KUMPONGEZA MHE. DR. TULIA ACKSON MWANSASU (MB) NAIBU SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA 13/6/2016.


Ndugu wana habari na watanzania mnao tufuatilia kupitia redio na televisheni tupo hapa mbele yenu kwa lengo mahususi la kumpongeza Mhe. Dr. Tulia Ackson Mwansasu (MB) Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayo ifanya katika kuliongoza na kulisimamia Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa umahiri na ueledi na wa hali ya juu.

Watanzania wote ni mashahidi kwa namna ambavyo Mhe. Dr. Tulia Mwansasu anavyo lisimamia na kuliongoza Bunge letu kwa kuzingatia sheria, kanuni, na maadili ya Bunge na hivyo kurejesha heshima, nidhamu na uwajibikaji kwa Wabunge katika utekelezaji wa majukumu yao ya kuwawakilisha wananchi.

Kwa mfano hivi karibu tumeshuhudia akitoa mwongozo wa kutokulipwa fedha Wabunge wanaoingia Bungeni na kutoka mara tu baada ya kujisajili pasipo kutimiza wajibu wao hasa kwa kuzingatia kuwa HAKI na WAJIBU vinakwenda pamoja.

Vile vile kipekee kabisa na kwa umuhimu mkubwa UVCCM Mkoa wa Mbeya & Songwe tunapenda kumshukuru Mhe. Rais wetu Mpendwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kwa kumteua Mhe. Dr, Tulia Mwansasu (MB) kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kisha kuteuliwa na CHAMA CHA MAPINDUZI kuwa Mgombea pekee wa nafasi ya Unaibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye kuaminiwa kwa kuchaguliwa na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kura nyingi na za kishindo.

Sanjali na hivyo tunapenda kumpongeza Mhe. Rais wetu Mpendwa Dr. John Pombe Magufuli kwa hatua mbali mbali anazo endelea kuzichukua katika kutuletea Maendeleo Wananchi wa Tanzania ikiwa ni pamoja na kupiga vita rushwa kwa vitendo. Pia tunawashukuru na kuwapongeza sana Waheshimiwa wabunge wote wanao tokana na CHAMA CHA MAPINDUZI Kwa Kazi kubwa wanayo endelea kuifanya katika kuisimamia na kuishauri serikali ,UVCCM Mbeya & Songwe tunawashukuru sana kwa namna ya kipekee wanavyo endelea kumpatia ushirikiano wa kutosha Mhe. Rais wetu mpendwa na Mhe, Naibu Spika wetu Mungu awabariki.

Tunasikitishwa na kulaani vikali vitendo vinavyo fanywa na Wabunge wa Upinzani vya kutaka KUMHUJUMU Mhe, Naibu Spika kwa sababu zao binafsi zisizo na maslahi kwa Umma isipo kuwa kwa vyama vyao pekee kwani huwezi kumuundoa Mhe, Naibu Spika kwa kusimamia kanuni na taratibu zilizo tungwa na wao wenyewe waheshimiwa Wabunge na kuwanyima wananchi walio wachagua haki yao ya msingi ya kuwawakilisha kwa kususia vikao vya Bunge kwa kisingizio cha kutokuwa na IMANI na Naibu Spika ili hali lengo lao ni kuhakikisha wanapata nafasi ya kuendeleza mizaha na siasa zisizo na tija kwa Taifa letu ndani ya Bunge kwani nidhahiri kuwa hivi sasa Wapinzani wamekosa Ajenda za kuzisimamia baada ya vyama vyao kuwakaribisha na kuwakumbatia Mafisadi pia kwa kazi nzuri inayofanywa na Mhe, Rais ya kutatua kero za Wananchi kwa kiwango kikubwa. Na zaidi sifa, uwezo na uweledi alionao Mhe, Naibu Spika Dr. Tulia Ackson Mwansasu vinavyomuwezesha kulisimamia na kuliongoza Bunge kikamilifu ikumbukwe Mhe, Dr, Tulia Ackson Mwansasu ni msomi na mbobezi wa sheria kwa kuzisoma, kuzifundisha, kuziandika na kuzifanyia kazi hivyo Mhe, Naibu Spika anachokifanya ni kuzisimamia na kuzitekeleza sheria na kanuni za Bunge zilizotungwa na Bunge na hakuna kanuni mpya alizokuja nazo Mhe, Naibu Spika, kama Wapinzani wanavyotaka kuwaaminisha Wananchi.

UVCCM Mbeya & Songwe tunasema Usirudi nyuma Mhe. Dr. Tulia Ackson Mwansasu watanzania wengi tupo nyuma ya kazi yako njema na yenye maslahi kwa Taifa.
RAI YETU KWA WAPINZANI.

Tunawashauri Ndugu zetu wa upinzani kurejelea maneno ya busara tuliyo kumbushwa hivi karibuni na Waziri wa sheria na katiba Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe (MB) kutoka kwa Mwana falsafa nguli wa Ugiriki “PLATO” aliye pata kusema “wenye busara husema wanapokuwa na kitu cha kusema, wapumbavu husema ili mradi waseme chochote”. Ni dhahiri kwamba Wapinzani hawana cha kuwaambia Watanzania kwa muda huu hivyo sio muda muafaka kwao kutaka kuzunguka nchi nzima kuwahadaa wananchi. Hata hivyo upinzani wanatakiwa kulishukuru sana jeshi la Polisi kwa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa kwani kwa kufanya hivyo limewaondolea aibu kubwa ambayo wangeipata kwenye Ziara yao kwa kupuuzwa na wananchi.

Tunawataka wabunge wa upinzani warejee Bungeni kuwawakilisha wananchi walio wachagua kwa kuwatetea kwa hoja za msingi zenye maslahi kwa Taifa na sio vyama vyao pekee.

Vivyo hivyo tunawaomba upinzani kubadilisha matumizi ya fedha walizokuwa wamepanga kuzitumia kuzunguka nchi nzima, badala yake wazipeleke kwenye ununuzi wa Madawati kwenye majimbo yao ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Mhe Rais Dr. John Pombe Magufuli katika kukabiliana na uhaba wa Madawati nchini.

Mwisho japo sio kwa umuhimu UVCCM Mkoa wa Mbeya na Songwe tunawatakia waislam wote wa Tanzania mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan na tunawaomba watanzania wote tuwape ushirikiano Ndugu zetu katika wakati huu muhimu kwa kutenda matendo mema yampendezayo Mwenyezi Mungu.

MUNGU IBARIKI MBEYA NA SONGWE, MUNGU MBARIKI MHE. DR. TULIA ACKSON MWANSASU MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 Asanteni kwa kutusikiliza.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Imetolewa na Amani L. Kajuna.

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya & Songwe.