Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, June 19, 2013

AHUKUMIWA MIAKA 30 BAADA YA KUKIRI KUMPORA ASKARI MAGEREZA BUNDUKI

 Ali Salum (32) ambaye ni mshtakiwa namba moja amekiri kosa lake la kupokonya siraha na amehukumiwa kutumikia kifungo kwa miaka 30
Braison Sanga yeye ni mtuhumiwa wa 3 baada ya kuona mwenzake amefungwa miaka 30 nae akaamua kukiri kosa lake kuwa yeye ndiye aliekuwa napanga wakati wa kupokonya siraha hiyo
Hili ndilo panga lililotumika kumkata askari magereza wakati wa kumpokonya siraha yake
Hii ndiyo siraha aliopokonywa askari huyo watuhumiwa waliifunga kwenye mkeka
askari WDR Ambrose akitinga mahakani kusikiliza hukumu ya watuhumiwa wake

Watu wanne  wamefikishwa Mahakamani wakituhumiwa kutenda kosa la kufanya unyang’anyi wa kutumia Silaha kwa kumpora Askari Magereza Bunduki na hukumu ikitolewa kwa Mshtakiwa mmoja ambaye amehukumiwa miaka 30 jela.
  
Mwendesha Mashtaka wa Serikali Mwajabu Tengeneza akisoma Mashtaka Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya Aneth Nyenyema amesema Washtakiwa wote wanne  kwa pamoja walitenda kosa hilo kinyume cha Sheria ya kanuni ya adhabu kifungu cha 287(A) sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
  
Amewataja watuhumiwa kuwa ni Ali Salum (32) ambaye ni mshtakiwa namba moja akiwa na Emmanuel Martin(25), Braison Sanga na John Waziri(22) ambao ilidaiwa kuwa Mei 5, Mwaka katika eneo la Magereza Songwe walimvizia askari WDR Ambrose na kumjeruhi kisha kumpokonya bunduki aina ya SRA yenye namba za usajili TZ PS 39847164020 mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kitengo cha Jeshi la Magereza.
  
Kutokana na Mashtaka hayo watuhumiwa wote walikana isipokuwa Mshtakiwa namba moja ambaye alikubali kutenda kosa hilo hali iliyomlazimu Mwendesha mashtaka kumsomea mara tatu ili kujua kama ameelewa mashtaka yake.

Na Mbeya yetu


1 comment:

Anonymous said...

silaha siyo siraha ndungu yetu, kiswahili ni lugha yako.