Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, July 25, 2013

SHUKURANI KUTOKA TGNP KWA WAANDISHI WA HABARI

25.07.2013

YAH: KUSHIRIKI NA KUCHANGIA KWAKO KATIKA WARSHA YA WAANDISHI WA
HABARI ILIYOFANYIKA MWEZI MEI, 2013.
Saalam toka TGNP Mtandao,
Mpendwa katika harakati za ujenzi wa vuguvugu la kuwakomboa wanawake
kimapinduzi, tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ushiriki wako katika
warsha ya waandishi wa habari iliyofanyika mwezi Mei, 2013 katika mikoa ya Mbeya,
Morogoro na Shinyanga.
Tunashukuru pia kwa kuendelea kutumia kalamu zenu kama sehemu ya kupaza
sauti kudai na kupigania haki za wanawake na wanaume hasa walioko pembezoni,
katika kufikia usawa kwa kupambana na mifumo kandamizi ambayo imekuwa
ikiendelea kuwanyonya,kuwanyanyasa, kuwakandamiza na kuwabagua wanawake
na kushindwa kufikia malengo na ndoto zao katika kupata maisha endelevu na
maendeleo kwa ujumla.
Tunaamini kuwa ahadi yako uliyotoa wakati wa warsha itasaidia sana kuwa sehemu
ya kufuatilia, kuchambua, na kuendelea kutoa sauti katika kero mbali mbali
zilizoibuliwa wakati wa mafunzo ya kiraghbishi yaliyofanyika katika baadhi ya Kata
zilizofikiwa lakini pia katika kufuatilia masuala yanayowagusa wanawake na
wasichana kwa mtizamo wa kuwakomboa wananchi wote hasa wanawake na
wanaume walioko pembezoni ndani na nje ya nchi ili kuleta mabadiliko chanya.
Tunaamini kuwa tutaendelea kufanya kazi pamoja kwa kutumia kalamu zenu katika
kuchangia na kuleta mabadiliko ya kuwakomboa wanawake na wanaume hasa
walioko pembezoni
Wako katika mshikamano,
Kenny Ngomuo,

k.n.y Mkurugenzi Mtendaji -TGNP

No comments: