Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, September 12, 2013

DC RUNGWE CRISPIN MEELA ATUNUKIWA CHETI CHA HESHIMA.

Mkurugenzi wa Chuo cha Biashara na Utalii(HAOB) kilichopo Kiwira Wilayani Rungwe,Hanish Chunda akimtunuku cheti mkuu wa wilaya Rungwe Crispin Meela

 Katibu tawala wa Wilaya Rungwe, Alinanuswe Mwalufunda, amesema kitendo kilichofanywa na uongozi wa Chuo ni kitendo cha kuigwa kutokana na kutambua mchango wa viongozi wao tofauti na wengine ambao wanashindwa kutoa shukrani kwa kazi wanazofanyiwa.
Tumaini Emanuel akisoma risala 
 Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Crispin Meela amesema Kiongozi yeyote hawezi kujitathimini yeye mwenyewe kutokana na utendaji kazi wake isipokuwa jamii anayoiongoza ndiyo inayoweza kusema lolote kama ni mtendaji kazi mzuri ama mbovu  lakini siyo kusimama na kujigamba mbele za watu.
Picha ya pomoja

MKUU wa Wilaya ya Rungwe, Crispin Meela, ametunukiwa Cheti cha Heshima cha Stashahada ya Kwanza(Advance Diploma) na Chuo cha Biashara, Hoteli na Utalii baada ya kutambua mchango wake katika jamii na Wilaya kwa Ujumla.


Akizungumza wakati wa kumkabidhi cheti hicho katika Hafla iliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Mkurugenzi wa Chuo cha Biashara na Utalii(HAOB) kilichopo Kiwira Wilayani Rungwe,Hanish Chunda amesema wamelazimika kufanya hivyo baada ya kutambua mchango wake kutokana juhudi anazozifanya katika Wilaya ya Rungwe.


Chunda amesema moja ya sababu iliyofanya Chuo chake kumtunuku cheti Mkuu wa Wilaya ni pamoja na juhudi zake za kuimarisha hali ya utulivu katika Kata ya Kiwira kutokana na eneo hilo kukithiri kwa vitendo vya vurugu na matukio ya kutisha lakini hali sasa ni nzuri baada ya Mkuu huyo kusimamia na kuhakikisha hali ya amani inarejea.


Amesema kutokana na kutulia kwa eneo hilo kumeongeza fursa nyingi za uwekezaji wa Biashara Elimu na Kilimo baada ya watu kuondolewa hofu na kuridhika na hali ilivyo ambapo hadi wao wakalazimika kujenga Chuo cha Biashara katika maeneo hayo ya Kiwira na kuishi kwa amani na wakazi wanaozunguka Chuo.


Amesema Cheti hicho ni moja ya kushukuru kutokana na ushiriki wake katika shughuli za chuo hicho tangu kinaanzishwa mwaka 2009 ambapo alipata nafasi ya kuweka jiwe la msingi katika eneo lililotolewa na wananchi wa kijiji cha Ilundo kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha Biashara na utalii jambo linalodhihirisha wazi kuwa anapenda maendeleo ya elimu kwa wananchi wa Kiwira.

Ameongeza kuwa pia ameshiriki kuwa mgeni rami katika Mahafali ya tatu ya chuo hicho yaliyofanyika April 25, Mwaka huu pamoja na kukubali kuwa mlezi wa Chuo hicho kwa kuonesha dira na moyo thabiti wa kusimamia shughuli za Chuo ili kuendena na matakwa ya Serikali ya kumkomboa Mwananchi wa chini kielimu.


Akitoa shukrani kwa niaba ya Watumishi wa Wilaya ya Rungwe, Katibu tawala wa Wilaya hiyo, Alinanuswe Mwalufunda, amesema kitendo kilichofanywa na uongozi wa Chuo ni kitendo cha kuigwa kutokana na kutambua mchango wa viongozi wao tofauti na wengine ambao wanashindwa kutoa shukrani kwa kazi wanazofanyiwa.


Amesema kama Wilaya kuwa na viongozi ambao jamii inatambua mchango wake ni jambo la kujivunia na kuongeza juhudi na kumpa ushirikiano ili matunda yake yazidi kuonekana katika kuwaletea maendeleo wananchi ikiwa ni pamoja na watumishi wengine kufanya kazi kwa bidii ili kuiga mfano.


Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Crispin Meela amesema Kiongozi yeyote hawezi kujitathimini yeye mwenyewe kutokana na utendaji kazi wake isipokuwa jamii anayoiongoza ndiyo inayoweza kusema lolote kama ni mtendaji kazi mzuri ama mbovu  lakini siyo kusimama na kujigamba mbele za watu.


Amesema kitendo cha chuo hicho kumpongeza ni kitendo cha kuigwa na kutambua mchango wa Serikali na Ofisi ya Wilaya kwa ujumla na siyo yeye binafsi na kutoa Wito kwa jamii kushirikiana ili kuwaletea maendeleo Wananchi ikiwa ni pamoja na kufuata misingi na Sheria za nchi ili kudumisha amani.


Amesema kupungua kwa vitendo vya uhalifu katika Wilaya ya ni kutokana na Serikali kuchoshwa na sifa mbaya iliyokuwepo na kuapa kulivalia njuga kwa nguvu zote kwa kuwakamata wanaohusika na vitendo hivyo ili wanaobaki kupata woga wa kurudia au kuiga kufanya maovu ndani ya Wilaya hiyo.

Na Mbeya yetu

1 comment:

Anonymous said...

CERTIFICATE OF EXELLENT...
ADVANCE DIPLOMA....

kingereza hiki ni muhimu kufanyia editing jamani....na hicho ni chuo je kwingineko haki ikoje