Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, August 12, 2013

SALAMU MAALUM ZA SHUKURANI KUTOKA MBEYA YETU BLOG BAADA YA KUPATA USHINDI WA KUWA CHOMBO BORA KATIKA MATANGAZO YA DIGITALI WAKATI WA MAONESHO YA NANE NANE KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI MBEYA.

Hii ndiyo hati ya Ushindi tuliyopewa na TASO
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawilo aliye simama Mbele akipokea Maelezo ya Kina juu ya Mbeya yetu Blog inavyofanya kazi na mitandao mbalimbali ya Kijamii kutoka kwa Mtaalam wa Mambo ya Mitandao ya Digitali kutoka Tone Multimedia Group Fredy Anthony, alipo tembelea katika Banda la Mbeya Yetu Blog.
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh. Dr. Christine Ishengoma aliyevaa kofia akipokea Ufafanuzi wa Jambo Kuhusu Blog ya Mbeya yetu kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa Mtandao wa Mbeya yetu Ambaye Pia ni mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Tone Multimedia Ndugu Joseph Mwaisango wa Pili kutoka Kushoto
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. Christine Ishengoma akitaka kupata ufafanuzi wa jinsi gani Mbeya yetu Blog tunavyopata habari na kuziweka kwa Muda kama alivyo kuta tukio lake likiwa Live mara alipotembelea Banda la Mbeya yetu na kujionea mwenyewe.
Kutoka Kushoto ni Venance Matinya na David Nyembe wote kikosi kazi cha Mbeya yetu Blog, wakiwa wanapita Mbele kuonesha Bango la Mbeya yetu kwa Mgeni Rasmi wakati wa sherehe za Kilele cha siku  ya Wakulima Nane nane Mbeya.
 Msimamizi Mkuu wa Mtandao wa Mbeya yetu Ambaye Pia ni mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Tone Multimedia  Ndugu Joseph Mwaisango akipokea Hati ya Ushindi kutoka kwa Mgeni Rasmi aliyevaa Skafu Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Capt (RTD) Aseri Msangi 
Baadhi ya kikosi kazi cha Mbeya Yetu Blog, Kutoka kushoto ni Venance Matinya, Joseph Mwaisango, Ezekiel Kamanga na Fredy Anthony

 ********************
Chama Cha Wakulima Tanzania (TASO) kanda ya Nyanda za juu Kusini, kimeutunuku cheti mtandao wa kijamii wa www.mbeyayetu.blogspot.com ambao upo chini ya Tone Multimedia Company Limited kutokana na kuibuka mshindi wa kwanza wa kurusha matangazo kwa njia ya Kidigitali katika maonesho ya Wakulima nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya John Mwakagale Uyole Jijini Mbeya.
Tuzo hiyo imekuja kutokana na kikosi cha Mtandao huu kuweka kambi katika maonesho hayo na kufanya shughuli za kurusha matangazo moja kwa moja kutoka uwanjani hapo na kuwapagawisha wakulima ambao walipata fursa ya kutembelea banda letu na kujionea habari zilizotokea muda huo huo na kuonekjana hewani.
Mbali na wakulima na watu mbali mbali waliokuwepo uwanjani hapo pia viongozi wa Taso na wakuu wa Mikoa pia walipata fursa ya kutembelea banda la Mtandao huu katika ziara zao za kukagua mabanda na hivyo kutoa sifa kwa wamiliki wa Mtandao huu namna habari zilivyokuwa zikienda kwa wakati.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawilo ndiye aliyekuwa wa Kwanza kufanya ziara hiyo na kukuta habari zake tokea akipokelea mlangoni hadi kufikia mabanda habari zilikuwa hewani, mwingine alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dr. Christine Ishengoma ambaye pia alionekana kuufagilia mtandao huu kwa namna walivyoweza kutangaza Nanenane  iliyofanyika kikanda na kuonekana kama ni Kitaifa.
Aidha kufuatia mchango huo wa Taso na wakulima kwa ujumla Uongozi wa Tone Multimedia Group Kupitia  Mbeya Yetu Blog unatoa shukrani kwa wote waliuofanikisha shughuli za Nanenane hadi zinafikia kilele Agosti 8,  na kupelekea kupata cheti cha ushindi.
Tunapenda kuwashukuru TASO kwa namna ya pekee, SBC (T) Ltdkupitia kinywaji chao cha Pepsi, Shirika la Bima ya Afya (NHIF) kwa kutupatia gazebo lililotusitili tukiwa kazini na wengine wengi ambao hatutaweza kuwataja majina lakini tunaahidi kuendelea kushirikiana kwa pamoja.

Pia tunapenda kuwashukuru Bloggers wote na waandishi wa habari kwa ujumla hatutaweza kutaja kila chombo lakini tumekuwa pamoja mpaka kufanikisha yote haya.

Mwisho kabisa Tunapenda kukushukuru wewe Mdau wetu Mkubwa wa Mbeya yetu Blog kwa kuonesha Moyo na Kutembelea kila wakati mtandao huu, Tunasema asanteni sana, Bila nyie sisi hatuwezi fanya kazi.
KWA PAMOJA TUUPENDE MKOA WETU WA MBEYA, KUPITIA MTANDAO WA MBEYA YETU BLOG.

No comments: